Jarida la Wanafunzi wa Kiswahili

      Toleo la pili (Fall 97). Someni kwa furaha!

      ==========================================================

      K W A N Z A A

      na Tonyardzwa Taylor, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza

      Kwanzaa Yenu Iwe Na Heri!

      Kwanzaa ni sherehe ya "African-Americans". Tunashangilia uhai Dr. Maulana Karenga, mwalimu mkuu za historia "African-American" katika chuo kikuu cha California alianzisha Kwanzaa mwaka 1966. Kwanzaa inasherehekewa kwa muda waa siku saba, kutoka Desemba ishirini na sita mpaka Januari moja, kwa kufuata nguzo saba. Nguzo hizi saba ni:

      1. Umoja (Unity)
      2. Kujichagulia (self-determination)
      3. Ujima (collective work and responsibility)
      4. Ujamaa (cooperative economies)
      5. Nia (purpose)
      6. Kuumba (creativity)
      7. Imani(faith)

      Pia kuna alama saba:

      1. Kikombe cha Umoja (Unity cup): Tunakunywa kutoka kikombe cha umoja
      2. Kinara (candle holder): Kinara kinashika mishumaa
      3. Mazao (fruit)
      4. Mkeka (straw mat)
      5. Mishumaa Saba (seven candles)
      mishumaa mitatu ina rangi kijani yenye Maana ya matumaini
      mishumaa mitatu ina rangi nyekundu yeny maana ya kupigania uhuru
      mshumaa mmoja una rangi nyeusi yenye maana ya umoja wa watu weusi
      6. Mahindi (ears of corn) ni dalili ya watoto na maendeleo
      7. Zawadi(gifts)

      Unaweka Kinara juu ya Mkeka. Mishumaa saba inafanana na nguzo saba. Unawasha mshumaa mmoja kila siku. Unaanza kwa mshumaa mweusi. Siku ya pili unawasha mshumaa wa kushoto, siku ya tatu unawasha mshumaa wa kuume. Chakula cha sherehe ya Kwanzaa, jina lake ni Karamu. Kwa kawiada inaanza tarehe thelathini na moja Desemba. Jamaa wanasimulia nguzo ya siku na wanatoa mawazo yao juu ya nguzo hii. Baada ya kuwasha mishumaa, jamaa wanafanya ukumbusho wa watu wa kale. Wanankuywa kutoka kikombe cha Umoja. Baada ya kunywa, wanainua juu kikombe cha umoja na wanasema "harambee". Maana ya ÒharambeeÓ ni "let's pull together". Tunakula viazi vitamu, mchuzi wa mboga, keki za kunde, na mabamia ya kukaanga.

      *************************************

      BENDERA ZA AFRIKA

      na Noelle Lee (Mwihaki), mwanafunzi wa mwaka wa kwanza

      Katika Afrika kuna bendera hamsini na tatu; bendera moja kwa kwa kila nchi ya Afrika. Bendera za Afrika zina rangi ya kijani, na rangi nyekundu, na rangi ya manjano. Rangi nyeupe na rangi nyeusi zinatumia sana pia. Alama za nyota na mwezi zina maana maalum. Mistari inatumiwa sana pia.

      Bendera ya Uganda ina rangi nne: rangi nyeusi na rangi nyeupe, na rangi ya manjano na rangi nyekundu. Ina mistari ya rangi nyeusi na rangi nyekundu na rangi ya manjano. Ina duara la rangi nyeupe na ndege wa rangi nyekundu na rangi nyeupe.

      Bendera ya Libia ni rangi ya kijani.

      Rangi za bendera ya visiwa vya Comoro ni kijani na kuna nyota nne na mwezi wa rangi nyeupe.

      Bendera ya Tanzania ina rangi nne: rangi ya buluu, rangi ya manjano, rangi nyeusi, na rangi ya kijani.

      Bendera ya Algeria ina rangi mbili - rangi nyekundu na nyota na mwezi wa rangi nyeupe.

      Kwa kawaida, rangi za bendera zina maana maalum. Rangi ya buluu, kwa mfano, ina maana ya maji. Nyeusi ni rangi ya watu, na ina maana ya nguvu za taifa. Rangi ya manjano ina maana ya madini au, hasa, dhahabu. Mara kwa mara, silaha ni alama ya nguvu na uhuru. Ninafikiri ndege ni alama ya uhuru pia.

      Bendera ya Liberia na bendera ya Afrika ya kusini ni tofauti na bendera nyingine. Bendera ya Liberia ina rangi nyekundu na rangi nyeupe na rangi ya buluu. Rangi sawa na bendera ya Amerika. Bendera ya Liberia ina mistari ya rangi nyeupe sita na rangi nyekundu tano. Bendera ya Amerika ina mistari ya rangi nyeupe sita na mistari wa rangi nyekundu saba. Bendera ya Amerika ina nyota hamsini lakini bendera ya Liberia ina nyota moja. Bendera ya zamani ya Afrika ya kusini ni kama bendera ya Ufaransa na Uingereza.

      ************************************

      KUSOMA KISWAHILI TANZANIA

      na Stacey Langwick, mwanafunzi aliyeendelea

      Kijifunza Kiswahili katika chuo kikuu cha Pennsylvania ni vizuri, lakini kusoma kisawili katika Tanzania ni vizuri zaidi. Kiangazi hiki nilienda Tanzania pamoja na Group Project Abroad Program inayofundisha na chuo kikuu cha Yale. Darasa hilo linafundishwa kila mwaka kwa wiki nane tu, lakini wanafunzi hujifunza mambo mengi. Wanafunzi wote ambao husoma katika darasa hilo walisoma Kiswahili kwa muda wa miaka miwili au mitatu kabla ya kushiriki katika programu hii.

      Mwaka huu, darasa la Kiswahili lilifundishwa katika Arusha na Unguja. Katika Arusha, walimu wanne wanaotoka Dar es Salaam walikuja kufundisha wanafunzi kumi na mbili. Katika Unguja, wanafunzi hao walifundishwa na walimu wanaofanya kazi Tasisi ya Kiswahili na lugha za kigeni. Kulikuwa na walimu wengi kwa wanafunzi wachache tu. Kwa sababu hii, kila mwanafunzi alipata msaada wa kutosha. Mazingira hayo ni mazuri kusoma lugha mpya. Pia, wanafunzi walisoma Kiswahili katika darasa kwa muda wa saa tano kila siku. Baada ya kusoma Kiswahili, wanafunzi walihitaji kusema Kiswahili katika mji. Kama wakitaka kununua stampu au kadi au kinywaji, wanahitaji kusema Kiswahili. Kwa wiki nne katika Arusha, kila mwanafunzi alikaa pamoja na jamaa inayotoka Kimondolo, kijiji karibu na Arusha. Ninafikiri kwamba kukaa mahale ambapo unahitaji kusema Kiswahili wakati wote ni njia nzuri zaidi ya kujifunza Kiswahili kuliko njia nyingine yoyote.

      Sehemu mbili bora za darasa hilo zilikuwa kukaapamoja na jamaa karibu na Arusha na kufanya utafiti kuhusu utamaduni katika Unguja. Nilipenda kukaa na jamaa inayoishi Kimandolo kwa sababu niliweza kuzungumza kuhusu vitu muhimu kwa watu wanaoishi Tanzania; niliweza kusikiliza watu wengi wanaosema Kiswahili; na niliweza kuuliza maswali mengi. Kwa mfano, nilizungumza kuhusu dawa ya kinyeji na babu anayeishi ndani ya nymba ambayo nilikaa. Pia, nilizungumza na mama kuhusu biashara na baba kuhusu siasa. Nilizungumza na mama mdogo kuhusu mambo mengi kutoka uzazi wa mpango mpaka mapishi. Nilisomia hadithi mtoto mdogo na watoto wakubwa walinisaidia kazi yangu ya nyumbani. Katika mazingira haya nilijifunza Kiwahili kingi, pia nilianza kujifunza kuhusu njia kusema vitu fulani na wakati gani ulikuwa nzuri wakusema vitu hivyo.

      Pili, katika Unguja nilifanya utafiti kuhusu chakula cha Kisiwa cha Unguja. Nilianza kuandika kitabu cha mapishi katika Kiswahili. Nilichagua utafiti huu kwa sababu nilitaka kuzungumza na wanawake. Kwa kawaida, wanawake wanaoishi Unguja hawaendi pahale ambapo wageni wanawezi kuona kwa urahisi. Wanawake na wanaume wana kazi tofauti. Wanawake wanatumia muda mingi zaidi wa familia. Kwa hivyo, nilianza kufanya utafiti wangu pamoja na mama aliyekuwa na duka dogo nyumbani kwake. Kwanza, nilienda dukani kwake. Nilikaana nilizungumza na mama na jamaa yake na rafiki zake. Tulizungumza vitu vingi. Nilkwenda dukani kila siku. Baada ya siku chache, mama alinikaribisha jikoni kupika vyakula pamoja na familia yake. Pia, nilisema na wanawake wengine niliokutana nao kuhusu mapishi.

      Vilevile, kila jioni nilienda Darajani, kwenye bustani karibu na bandari ambapo wanaume na vijana wanakuja kupika na kuuza vyakula tofauti vya Unguja (kama kababu, pwezi, chapati, katlesi, na sambusa) na vinywaji tofauti (kama maji ya mua na chai ya mchaichai). Watu wengi -- wazanzibari na wageni, wanawake na wanaume, watoto na watu wazima -- huenda Darajani kila jioni kula na kukaa karibu na maji. Mahale bora kujifunza Kiswahili ni Tanzania. Kama ukisoma Kiswahili kwa miaka miwili au mitatu, unaweza kuandika maombi kuenda Tanzania pamoja na chuo kikuu cha Yale. Baada ya kurudi, utajua zaidi kuhusu Kiswahili, kuhusu utamaduni wa waswahili, na kuhusu mazingira ya uswahili.

      **************************************

      MCHEZO WA MANENO:

      Maneno gani yenye herufi nne au zaidi unaweza kuyatoa kwenye neno KISWAHILI?

      Maneno : akili, asili, hila, hili, hiki, hisi, hisa, haki, hali, halii, halisi, hawi, hiliki, hawahi, iliki, kiasi, kasi, kali, kaki, kila, kisa, kili, kisiwa, kiwili, liwa, lisha, lasi, laki, likisha, lia, sali, sala, sili, siki, sikia, siwi, siwahi, swali, shika, wahi, wali, wakili, wasili, wiki.

      Je, kuna maneno mengine? Niandikie.

      *************************************
      Toleo la kwanza

      Wanafunzi wa Kiswahili wa vyuo vingine wanaweza kumletea mhariri asomar@ccat.sas.upenn.edu makala mbali mbali ili zichapishwe katika toleo la tatu mwezi wa Mei, 1998

      Rudi ukurasa mkuu wa Kiswahili

      *************************************

      Last Modified: Machi 16, 1998
      Alwiya S. Omar, asomar@babel.ling.upenn.edu
      African Language Coordinator