Sehemu ya kwanza
Wakati ana umri wa miaka hamsini na tano, Majaliwa
alikuwa bado anafanya kazi ya ukuli. Kazi hii aliianza wakati yungali kijana wa
miaka ishirini na moja. Mazoea ya kazi hiyo yalimfany a aimudu vizuri
kabisa. Alikuwa mtu mashuhuri sana miongoni mwa wafanyakazi wa bandarini. Dongo la
Majaliwa lilikuwa zuri sana kwani hata katika umri wa miaka hamsini na
tano alionyesha kama kijana wa m iaka thelathini tu. Alikuwa na urefu wa
wastani na mwingi
wa
mwili.
| Majaliwa ailikuwa mwingi wa heshima, lakini pindi
alipokuwa kazini, aliziweka heshima hizo pembeni na kushika masihara na
matusi kama ilivyo tabia ya mkuli. Lakini palipotokea matatizo alikuwa ni
mtu wa busara na mwingi wa huruma. Mara kwa mara aliwanasihi wenzake
waliokabiliwa, na matatizo namna kwa namna hata ikawa kila walipokuwa na
matatizo ya kinyumbani, wafanyakazi wengi wa bandarini, walimhadithia
Majaliwa ili awape
nasaha na maongozi.
| Majaliwa alikuwa na mkewe aliyeitwa Mashavu. Ijapokuwa
Majaliwa na Bi Mashavu walioana walipokuwa vijana, kwa muda mrefu walikuwa
hawakubahatika kupata mtoto. Walikata tamaa ya kupata mtoto na hakuna
mzimu walioubakisha tokea Unguja hadi Pemba katika jitihada za kuomba
mtoto. Walipata mtoto wao wa kwanza na wa mwisho wakati wote wawili
wameshakuwa watu wazima. Siku aliyozaliwa mtoto huyo, furaha ya wazee
wawili hao ilikuwa haina kifani. Alikuwa mtoto mwanamume, wakampa jina la
Rashidi .
| Tokea kuzaliwa Rashidi, baba yake aliendelea kufanya
kazi yake iliyompatia maisha na kumlea Rashidi. Alikuwa hodari wa kuamka
alfajiri; ila siku
moja mpaka
saa moja na nusu alikuwa bado amelala, amejifunika shuka gubigubi.
| Mashavu alikuwa
jikoni, na kwa ajabu aliyoiona kwamba mumewe bado hajaamka
mpaka saa zile, ilimfanya arejee chumbani kumsikiliza mume wake. Alikuja
mbele ya mlango wa chumba chao na kusimama mbele. Alimtazama mumewe na alipoona hana dalili ya kuamka alimwuliza :
Sehemu ya pili
| "Leo huendi kazini? "
| "Siendi," alijibu Majaliwa huku akiwa bado yupo
kitandani.
| "Kwa nini?"
| "Ah! Wacha kunikera na mchukue huyo mtoto awache
kupiga makelele.
| Rashidi, ambae alikuwa bado mchanga, alikuwa amekwisha
kuamka, akawa analia kwa kelele
kubwa.
| Bi Mashavu alimbeba Rashidi ambaye mara alinyamaza
kulia, na hapo Bi Mashavu alianza kumwuliza tena Majaliwa: "Sasa bwana leo
kwa nini hutaki kwenda kazini?"
| "Si kama sitaki kwenda kazini, nataka sana; lakini leo
najahisi hali yangu naumwa umwa, nahisi kama homa na kizunguzungu."
| "Sasa si bora nikakutelekea maji ya moto ujimwagie labda
utapata nafuu?"
| "Haya," Majaliwa alijibu.
| Bi Mashavu alimfunga Rashidi katika ubeleko na hapo hapo
alirejea jikoni na
kuteleka maji
ya moto. Vile vile alipika uji wa mapande na kuujaza pilipili manga kwa
matu-maini kwamba huenda ukamsaidia mumewe kupata nafuu.
| Majaliwa alikuwa hapendi kulala bila ya kwenda kazini
kwa kuhofia mambo nyumbani yangekwenda mrama. Shillingi mbili ambazo
alizipata kwa kutwa zilitumika kwa matumzi ya nyumbani isibaki hata senti
moja. Na wala si kama pesa hizo zilitosha, bali ilimlazimu azifanye zitoshe.
| Maji ya moto yalipokuwa tayari, Majaliwa aliingia chooni
na kukoga na baada ya kumaliza alikunywa bakuli moja la uji wa mapande na
kurejea kitandani.
| "Sasa leo bwana nini shauri ?" Bi Mashavu aliuliza kutaka
kujua habari ya chakula cha siku ile ambayo mumewe hakwenda kazini.
| "Nitajikongojea hivyo hivyo mpaka hapo kwa Hajitumbo nikatafute
cho chote,"
Majaliwa alijibu huko yupo kitandani
amejifunika shuka gubigubi.
| Ilipofika saa nne, Majaliwa ilimbidi kutoka na hakusimama
mpaka kwa Hajitumbo. Haikuwa masafa marefu kutoka Mferejimaringo mpaka hapo na baada ya kufika tu alinunua
fungu la muhogo na papa mkavu na hiyo ilitosha kwa chakula cha siku ile. Ama
kwa Rashidi, unga wa mtaa ulikuwepo nyumbani na hicho ndicho kilichokuwa chakula
chake cha siku ile.
Sehemu ya Tatu
| Siku ya pili Majaliwa alijihisi mzima na kama kawaida yake
alfajiri aliamka. Alivalia magwanda yake na kwenda zake gatini ambako kazi
ngumu ilikuwa ikimngojea.
| Siku ile kulikuwa na kazi ya kuteremsha vyuma vya njia ya
reli iliyokuwa ikijengwa huko Tanganyika. Vyuma hivyo viliteremshwa Unguja
ili baadaye visafirishwe tena mpaka huko Dar es Salaam.
| Aliopoingia tu gatini, Majaliwa alikutana na Akida na bila
ya kusalimiana Akida alianza masihara, "Jana hatukukuona jee, mama etu alikzuia
nini ?"
| "Nilipigwa na homa ya ghafla," Majaliwa alijibu.
| "Ah, twambie kweli bwana," Akida alizidi kuendelea na masihara
yake.
| "Unataka nikwambie kweli?" Majaliwa nae alianza masihara.
"Nikikwambia kweli halafu utakasirika, kwani hujui kama mimi ni shemaji yako na
yeye nd'o alienizuia nisije kazini jana?"
| "Ha, ha, ha," Akida alicheka kwa kelele na kusema, "Ama mzee
weye unpenda kujigamba."
| Majaliwa na Akida walikuwa wamefuatana pamoja kwani wote
walikuwa katika kikundi kimoja.
| Meli ilikuwa imeshafunga gati, waendeshaji kreni wameshapanda
juu ya kreni zao, na mara harakati za kuteremsha vyuma zilianza.
| "Lete! Lete! Lete!" Shaabani, mkuu wa kikundi cha akina
Majaliwa alikuwa anamwongoza mwendeshaji wa kreni wakati vyuma vinateremshwa.
| Makuli walikaa kwa hadhari hapo chini wakkifungua chuma
kimoja baada ya kuteremshwa.
| Kila baada ya kuteremshwa, chuma hicho kilichukuliwa na
watu wanne na kupelekwa mpaka nje ya uwanja wa gati ambako vyuma hivyo
vilipangwa.
| Kazi hiyo ngumu ilimalizika kazi tu, Majaliwa hakusimama
mpaka kwake.
| Alipofika nyumbani alimkuta Rashidi kachafuka, kelele
nyumba nzima, analia huku Bi Mashavu amempakata anachochea mmoto jikoni
huku akimbembeleza:
Usilie, usilie,
| Ukaniliza na mie,
| Machozi yako yaweke,
| Nikifa unililie.
Sehemu ya Nne
| "Nini tena unamwacha
mtoto analia tokea saa ile?"
Majaliwa ambae alikuwa chumbani akivua nguo aliuliza kwa hamaki.
| "Ah, hata sijui kinachomliza mtoto huyu," Bi Mashavu
alisema.
| "Mynyonyeshe basi, labda ana njaa," Majaliwa aliamrisha.
| "Ntamnyonyesha vipi nami n'na chungu jikoni?" Bi Mashavu
alijibu akiwa naye kisha hamaki.
| Joto pamoja na moto wa jikoni ndiyo yaliyokuwa yamkimliza
Rashidi. Bi Mashavu hakuwa na wa kumsaidia, alikuwa peke yake ndani ya
nyumba; msaidizi wake alikuwa mumewe Majaliwa.
| "Njoo umchukue basi utoke nae nje labda atanyamaza
,"
alisema Bi Mashavu.
| Majaliwa alivua nguo zake za kazini na kuzitundika
juu ya kamba chooni, alijifunga shuka yake kiunoni na hapo tena alimchukua
Rashidi na kutoka naye nje.
| Majaliwa alikuwa akimpenda mwanawe, kwani huyo alikuwa
ni mwana mjukuu. Alitoka naye nje na kukaa barazani na baada ya kucheza
naye kwa muda mfupi Rashidi alilala. Hapo tena Majaliwa alipata nafasi
ya kwenda kugoga na kupumzika
kidogo.
| Majaliwa aliingia chumbani huku akimwacha Bi Mashavu
akipakua chakula.
| Ijapokuwa chumba hicho kilikuwa kidogo, Bi Mashavu
alikiweka katika hali ya usafi kabisa. Kitanda cha samadari kilichokwemo
humo kilitandikwa vizuri kwa shuka nyeupe iliyofumwa maua mekundu katikati.
Mlikuwa na viti viwili vya 'murscheya' vilivyokuwa na mito ya usumba ambayo
ilivishwa foronya safi nyeupe. Kila magharibi Bi Mashavu alikuwa na kawaida
ya kunyunyiza asumini
juu ya kitanda na baadaye kufukiza udi ambao ulileta
harufu nzuri ndani ya chumba hicho. Kila siku kanga safi zilining'inizwa
juu ya besera ya kitanda
na Majaliwa, baada ya kwisha kukoga tu, alivuta
moja ya kanga hizo na kujifunga kiunoni.
| "Bwana, chakula tayari," Bi Mashavu alimwambia Majaliwa,
aliyekuwa amejinyosha juu ya kitanda kile kilichotandikwa vizuri huku
amemlaza Rashidi uvauni pake.
| Bi Mashavu naye alikuwa amekwisha koga, amejifunga kanga
moja kifuani na moja amejitanda. Amejitia tarabizuna ananukia vizuri. Sinia
ya chakula iliwekwa katikati ya chumba na hapo tena Majaliwa na Bi Mashavu
walikaa juu ya mkeka na kuanza kula.
| Huo ndiyo uliokuwa wakati wao wa starehe. Bi Mashavu
amempakata Rashidi, Majailwa amejifunga kanga moja tu tumbo wazi.
| "Rashidi kawa mtundu siku hizi," Bi Mashavu alianza
mazungumzo, "leo nilimuacha hapo katikati kidogo tu mara namsikia yupo
nje, tokea amejua huko kutambaa imekuwa shida."
| Nd'o mwanarnume, lazima awe mtundu
," Majaliwa alisema.
| " Unajionaje hali yako leo, ile homa imepungua?"
Bi Mashavu aliuliza.
| "Leo sijambo khassa
," Majaliwa alijibu.
| Majaliwa alikuwa si mtembezi wa usiku, hatoki isipokuwa
ana haja muhimu kwa hivyo walipomaliza ula tu alitoka nje kupunga upepo na
hii ndiyo iliyokuwa kawaida yake kila siku.
Sehemu ya Tano
| Siku ya pili kazi ya kuteremsha vyuma vya njia wa reli
iliendelea. Kila chuma kimoja, kama kawaida, kilichukuliwa na watu wanne.
| "Chukua vizuri!" Majaliwa ambaye alikuwa nyuma kabisa
alimpigia kelele kuli mwenzake aliyeonyesha amelegea kidogo na ambaye alikuwa
kati.
| Walikibeba chuma hicho mpaka pale uwanjani vinapokusanywa
vyuma vyote. Wakati wa kukitua chuma hicho iliwabidi wote wakitue kwa
umoja wao.
| "Tayari, tayari?," aliuliza yule aliyekuwa nyuma kabisa
alimpigia mbele kisha akaamuru, "Haya tupa!"
| Wote walikitupa kile chuma lakini kwa bahati mbaya yule
aliyekuwa kati alichelewa kidogo na uzito wote wa chuma kile ukamwelemea
yeye begani na mfupa wa bega lake la kuume ukadata.
| "Aaaaa!" akaanguka huku akipigia kelele nyingi kwa
maumivu. Wafanyakazi wenzake na wengine waliokuwa karibu walimzunguka
huku wakijaribu kumsaidia mfanyakazi mwenzao aliyekuwa akipiga mikambe
kama mtu mwenye kukata roho. Pale pale alikwenda kuitwa mkuu
wa gati ambae alikuwa Mwingereza. Muda si muda alifikia pale alipo
majeruhi yule. Alimbonyeza bonyeza na kumfanya yule mfanyakazi
azidi kupiga makelele kwa maumivu na mara yule Mzungu akasema, "Sasa
peleka yeye nyumbani."
| "Tumpeleke nyumbani?" Akida aliuliza. "Lazima
tumpeleke hospitali, ameumia sana huyu," aliendelea.
| "Nani tapeleka yeye hospitali?" Yule Mzungu aliuliza.
| "Gari ya kampuni si ipo?" Wote waliopo pale walisema
kwa umoja wao.
| Yule Mzungu ambaye alikuwa amechutama huku akimgeuza geuza majeruhi yule
alisimama na kuwatazama wafanyakazi wale mmoja mmoja na kwa ukali
alisema, "Nyinyi hapana jua kama gari ya kampuni iko kazi mingi?"
| "Muhimu hiyo kazi au huyu mtu aliyeumia? Unafikiri
kazi muhimu kuliko maisha ya mtu?" Akida aliuliza kwa hamaki.
| "Hiyo hapana shauri yangu," alijibu yule Mzungu na bila
ya kumtazama yeyote katika watu wale waliokuwapo pale alikwenda zake.
| Makuli wote walipigwa na mshangao, hawakujua la
kufanya; mwenzao amelala chini mahtuti, kauli hana, amebakia kuugua tu kwa maumivu
makubwa aliyokuwa nayo.
| "Mie n'na shauri moja", Majaliwa alisem kwa ghafla, " tuchageni, na pesa
zitakazopatikana tutakodi gari tumpeleke hospitali."
| Hapana aliyepinga shauri lile na hapo hapo upatu wa maridadi
ulianza. Aliyekuwa na senti ishirini, aliyekuwa na senti hamsini,
almuradi kila mtu alitoa alichokuwa nacho. Kwa jumla zilipatikana
shilingi kumi na hapo hapo mmoja alitoka kwenda kukodi gari na baada ya
kupatikana gari hiyo majeruhi yule alipelekwa hospitali.
| Makuli wote waliona unyonge mkubwa kwa ajali iliyompata mwenzao siku
ile na walikuwa na hakika kwamba asingeiweza tena kazi ya ukuli.
| Majaliwa alirejea nyumbani na huzuni kubwa. Fikira zake
zote zilikuwa kwa yule mfanyakazi mwenzake ambaye maisha yake yalikwisha
potea kwa kazi ya shilingi mbili.
Sehemu ya sita
| Alipofika nyumbani hakusema na mtu ila aliingia
chumbani na kukaa juu ya kiti bila ya hata kuvua maguo yake machafu ya
kazini. Alikaa pale na kujikamata kichwa.
| Bi Mashavu alipigwa na mshangao kwani hii ilikuwa siyo kawaida
ya mumewe. Hakustahimili kule jikoni alikokuwapo akipika, alimfuatia
mumewe chumbani ambako alimkuta alijiinamia kichwa chake amekizamisha
ndani ya viganja vyake viwili vya mikono. Akamwuliza "Mbona hivyo leo bwana,
ile homa imekurejea nini?"
| "Sina homa, " Majaliwa aiijibu kwa sauti ya chini.
| "Sasa cha mno nini tena?"
| "Ah, mwenzetu mmoja ameumia sana leo kazini na sijui
hali yake namna gani hivi sasa."
| Bi Mashavu hakutaka kuendelea na mazungurnzo hayo kwani
alihisi akitaka kuyajua zaidi atamzidishia unyonge mumewe. Aliusindika
mlango wa chumba na taratibu alirejea jikoni na Rashidi wake mgongoni.
| Hii haikuwa ajali ya kwanza bandarini hapo, ajali
nyingi kama hizo na mbaya zaidi zilitokea. Katika ajali nyingine
wafanyakazi walipoteza maisha yao na wengine walibakia viwete maisha yao;
wengi katika wao wakiishia kazi ya kuomba. Wafanyakazi wa bandarini
hawakuweza kufanya lolote ila kulalamika tu.
| Siku nenda siku rudi Majaliwa aliendelea kufanya kazi
ya ukuli. Kila alipoendelea kukonga afya ilizidi kumpungua, lakini
hata hivyo ilirnlazimu kuendelea na kazi ili aweze kuendesha maisha yake
yeye, mkewe na mtoto wake.
| Majaliwa aliendelea na kazi ya ukuli mpaka ikamvunja
kabisa na hatimae alipatwa na ugoniwa wa kiarusi ambao ulimlaza kitandani mpaka kufa kwake.
Alifia hapo hapo
Mferejimaringo na makuli wengi walihudhuria maziko yake hapo Makaburimsafa.
| Baada ya kifo cha Majaliwa, Bi Mashavu ilimbidi afanye
kazi ili aweze kuendesha maisha yeye na mtoto wake Rashidi ambae sasa
alikuwa mkubwa. Hakuna kazi aliyoweza kuifanya isipokuwa kazi ya biashara ndogo ndogo
kama vile kupika maandazi, kupika mboga na biashara nyingine kama hiyo.
Rashidi alimsaidia mama yake katika kazi zake zote; siku nyingine
alitembeza mikate ya
kusukuma au maandazi na siku nyingine alitembeza mihogo ya kuchemshwa.
| Rashidi hakuweza kuishi katika hali hii na baada ya
kufikiri sana aliona bora atafute kazi ya kuweza kumsaidia yeye pamoja na
marna yake Bi Mashavu. Kazi ya kwanza aliyofikiria ilikuwa ni kazi ya
marehemu baba yake, kazi ya ukuli.
|
|