Kwenda shule. Going to school.

Rehema na Tina ni wanafunzi wa shule ya msingi. Wao wanasoma shule tofauti. Rehema anasoma shule ya msingi Mtakuja na Tina anasoma shule ya msingi Mburani.

Juma: Habari za leo Tina?

Tina: Salama tu. Kesho utakwenda shule saa ngapi?

Juma: Nitakwenda saa kumi na mbili asubuhi. Na nitarudi saa tisa mchana.

Tina: Kwa nini unakwenda shule mapema sana?

Juma: Kwa sababu tunafanya usafi wa mazingira kabla ya kuanza masomo. Baada ya kusafisha mazingira sisi hukaa kwenye baraza, halafu tunaenda madarasani.

Tina: Sisi pia tunafanya usafi wa mazingira. Kila darasa lina sehemu yake maalum ya kufanya usafi. Viranja na walimu wa zamu husimamia usafi wa mazingira na shughuli nyingine.

Juma: Kesho darasa lenu mtasoma masomo gani?